Ligi Kuu

TFF wathibitisha kuzipeleka Simba na Yanga Arusha.

Sambaza....

Shirikisho la soka nchini TFF limethibitisha kuwa michezo miwili ya nyumbani ya African Lyon dhidi ya Simba na Yanga itafanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid uliopo Jijini Arusha.

Afisa habari wa TFF Clifford Mario Ndimbo amesema wameshapokea maombi ya African Lyon kutumia uwanjan huo na kuridhia hivyo kuanzia mchezo wa Alhamis ya Disemba 20 utakaowakutanisha wao na Yanga utafanyika jijini Arusha.

African Lyon FC

Yanga SC

African Lyon FC

Yanga SC

Sambaza....


Sambaza....

Uwanja

Sheikh Amri Abeid

Taarifa

Tarehe Muda Ligi Msimu Mwisho
20/12/2018 4:00 pm TPL 2018-2019 90'

“Timu ya African Lyon iliomba michezo yake ambayo inahusisha mechi za Simba na Yanga kuchezwa kwenye uwanja tofauti na uwanja wa Taifa, na kubadilisha kupeleka mechi zao kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid na barua ya Disemba 4 ilikubaliana na ombi lao na kuweka bayana kwamba mchezo unaofuata watakaocheza na Yanga utachezwa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha,” amesema.

“Uwanja huo Kama unakumbuka ulitumika kwenye fainali ya FA mwaka huu ukiwakutanisha Mtibwa Sugar na Singida United hivyo tunaamini Kuwa una vigezo kutumika kwa ajili ya mchezo huo,” ameongeza.

Ukiondoa African Lyon timu nyingine ambayo ilibadilisha uwanja ni JKT Tanzania ambao walipeleka mechi zao kwenye uwanja wa CCM Mkwawani Jijini Tanga.

Sambaza....
Subscribe
Notify of

0 Maoni
Inline Feedbacks
Tazama Maoni Yote
0
Tungependa kupata maoni yako, tafadhali tuambiax
()
x