
Kiungo mshambuliaji wa pembeni wa Simba sc Rashid Juma amefanikiwa kujiunga na timu ya Polisi Tanzania kwa mkopo akitokea Simba katika usajili huu unaoelekea mwishoni.
Rashid Juma amejiunga na Polisi Tanzania kwa mkopo wa mwaka mmoja akikimbia Msimbazi kutokana na ufinyu wa nafasi ya kucheza mbele ya kina Luis Miquissone, Francis Kahata na Hassan Dilunga lakini pia maingizo mapya kina Charles Ilanfia, Benard Morrison na Cris Mugalu.

Rashid Juma ni zao la Simba B ambapo alifanya vizuri akiwa chini ya Mwalim Mussa Hassan Mgosi na kupelekea kupandishwa kikosi cha wakubwa kilichokua chini ya Patrick Auseems.
Akiwa Polisi atakwenda kuungana na Ramadhani Pires, Daruesh Saliboko pamoja na Shabani Haruna kwenda kuunda safu mpya ya ushambuliaji.
Unaweza soma hizi pia..
Tamu na chungu za dakika ya mwisho!
Ligi kwa ujumla ilikuwa ngumu na yeye kusisimua licha ya bingwa kupatikana mapema lakini kiwango cha ushindani kilikuwa kikubwa hadi dakika ya mwisho.
Hizi hapa mechi kali zakumalizia Ligi!
Binafsi hii ndiyo michezo mikubwa miwili ninayoiangalia kwa jicho la uoga kwa kuwa ina maamuzi na hatma ya timu. Fiston Mayele na George Mpole!?
Huyu ndiye mchezaji wangu wa msimu
Tuandikie jina lake na kwanini unadhani anastahili kuwa mchezaji bora wa msimu.
Kiungo wa Stars asajiliwa Ubelgiji!
Kiungo huyo amejiunga na timu hiyo kwa mkataba wa miaka mitatu na sasa atakua akitonekana katika Ligi Kuu ya nchini Ubelgiji maarufu kama Jupiter Pro League.