Tayari kikosi cha Simba kimeshaanza maandalizi ya kushiriki michuano hiyo huku wakiwa tayari wanajinasibu wameanza usajili mzito kuelelea mashindano hayo.
Lakini endapo Simba watapata sare ama kupoteza maana yake ndoto zao zakufika nusu fainali mwaka huu zitakua zimekufa rasmi bila kujali matokea ya Horoya dhidi ya Raja.
Simba si tu hawana alama lakini pia hawajafunga bao lolote mpaka sasa katika michuano hiyo hivyo mchezo wa Vipers unatarajiwa kuwa mgumu na wakufufua matumaini yao yakufuzu robo fainali ya Klabu Bingwa Afrika.
Michezo yote sita (miwili ya ndani) ni muhimu kwa Simba katika kuamua mbio zao za ubingwa dhidi ya Yanga lakini pia michezo mitatu ya Kundi D itaamua kama watafuzu tena na kwenda robo fainali ya Ligi ya Mabingwa.