Lakini Fei wa sasa amereje upya kwenye form yake nadhani ndio muda wa kuondoka sasa, kiufundi anachopaswa kufanya ni kuongeza uwezo wa kutafsiri mahitaji ya mchezo kutokana na muda na tukio.
Baada ya kufanikiwa kuwaondosha Burundi katika hatua ya awali sasa Tanzania inasubiri upangwaji wa makundi ili kuweza kuanza safari ya kufuzu kombe la Dunia nchini Qatar.
Kutakuwa na makundi 10, kundi letu litakuwa na timu nne, tutacheza mechi 6, tatu ugenini na tatu nyumbani. Mechi hizi zinahitaji mbinu za uwanjani na hata nje ya uwanja. Waokota mipira ni sehemu ya mashambulizi na ulinzi wa Stars.