Moja ya dhumuni kuu la tovuti yetu ni kusheherekea mafanikio ya watu ambao wanafanya vizuri katika ulimwengu huu wa soka kwa Tanzania. Hivyo basi zifuatazo ni Tunzo ambazo tovuti hutoa kwa Wachezaji, Makocha na Wadau wa mpira wa miguu. Unaweza kubofya kwenye maelezo zaidi ili kujua jinsi utaratibu ulivyokuwapata washindi na orodha ya waliowahi kushinda. Kuanzia Msimu wa 2019/20 Tunzo zetu zitakuwa na utofauti na ndizo zitatumika kwa misimu yote ijayo kwa vipengele vilivyotajwa.

Galacha wa Mabao (Mwezi)

Lengo ni kusheherekea mafanikio ya ufungwaji mabao, huangalia tu ni mchezaji gani ambaye amefunga idadi kubwa kupita wenngine ndani ya mwezi mmoja katika Ligi Kuu ya Tanzania bara kwa wanaume pekee.Hutolewa mara moja tu kwa mwezi. Ikiwa wachezaji wamefungamana magoli, mchezaji aliyecheza mechi chache ndio atakuwa galacha wa magoli. Pia ikiwa wamefungamana kwa idadi ya mechi, itaangaliwa mchezaji gani amechea dakika chache zaidi.

Galacha wa Mabao (Msimu).

Huangalia rekodi ya mchezaji yupi ni mfungaji wa Mabao mengi zaidi katika msimu mmoja wa Ligi Kuu ya Mpira wa miguu Tanzania bara kwa Wanaume tu. Ikiwa wachezaji wamefungamana magoli, mchezaji aliyecheza mechi chache ndio atakuwa galacha wa magoli. Pia ikiwa wamefungamana kwa idadi ya mechi, itaangaliwa mchezaji gani amecheza dakika chache zaidi.

Galacha wa Hat-Trick

Tunzo hii huangalia nani anaongoza kwa kufunga Hat-Trick nyingi katika ligi Kuu kwa msimu husika. Tumeanza kutoa Tunzo hii katika Msimu wa 2019/20.

Iwapo wachezaji watakuwa wamefungamana, tutaangalia idadi ya magoli katika mechi husika, na/au matokeo ya mechi husika

Timu ya Msimu

Itaangalia klabu ambayo imechukua ubingwa kwa msimu husika, na kutazama matokeo yake katika msimu huo kwa timu ambazo zinashika nafasi nne za juu kwa ujumla wa alama walizokusanya kwa misimu mitatu iliyopita pamoja na wakati huo. Timu mshindi itaamuliwa kwa takwimu tu.

Galacha wa Kandanda**

Tunzo hizi ni mahususi kwa wachezaji, wadau na makocha wa mpira wa Miguu wanaocheza Tanzania (Ligi yoyote) na Wachezaji Watanzania walio nje ya Tanzania wakicheza soka la kulipwa. Rasmi itaanza 2020, lakini imekuwa na majaribio kidogo mwaka 2019 kwa waliofanya vizuri 2018. Tunzo hii inaangalia mafanikio na ‘perfomance’ kwa mwaka mzima (Januari hadi Disemba) tu.