Mchambuzi wa mpira wa miguu, mwenye Shahada ya Ualimu. Martin amejiunga na timu ya kandanda toka mwaka 2017, moja kati ya wachambuzi wakongwe katika familia yetu.
Mwisho wa kila safari huwa kuna funzo kubwa ndani yake, na binadamu siku zote huimarika na kuwa bora kupitia mafunzo tunayoyapata katika safari zetu kwenye maisha. Safari ya michuano ya kombe la nchi wanachama wa Afrika Mashariki (CECAFA) iliisha jana kwa kushuhudia Kenya ikichukua kombe lile. Kenya kuchukua kombe lile...
Jana kulikuwa na mechi ya Manchester Derby, mechi ambayo ilikuwa inawakutanisha mahasimu wawili ambao msimu huu wanaonekana kama timu ambazo zinauwezo wa kuwa bingwa. Manchester City walifanikiwa kuvunja rekodi ya Manchester United ya kucheza michezo 41 bila kufungwa katika uwanja wao wa nyumbani, na kufanya washinde mechi 8 zote walizocheza...
Leo kuna mechi ambayo inashika hisia za watu wengi wapenda mpira duniani. Mechi hii inakutanisha timu ambazo zinaonekana bora kwa sasa katika ligi kuu ya England, na ndizo timu ambazo zinaongoza mbio za ubingwa wa ligi kuu ya England. Manchester City akiwa anaongoza kwa tofauti ya alama nane dhidi ya...
Michuano ya CECAFA inaendelea kwa kuzikutanisha timu za taifa za wakubwa za nchi wanachama na nchi waalikwa kutoka kanda tofauti na ukanda ukanda huu wa CECAFA. Michuano ambayo inahistoria kubwa sana katika ukanda wetu huu wa Afrika Mashariki na Kati na Afrika kwa ujumla. Ndiyo mashindano yenye umri mrefu, kitu...
Inawezekana mafanikio ya Zidane yakawa yanakuja bila kelele yoyote kitu ambacho kinaweza kikashtua na kuona kama Zidane siyo kocha mkubwa . Vikombe sita ndani ya miaka miwili ni mafanikio makubwa sana kwake ingawa mafanikio haya yamekuja bila kelele yoyote. Kuna uwezekano mkubwa Bale, Benzema na Isco wakacheza katika kiwango kikubwa...
Njia ipi waliitumia Prisons kushambulia? Walipokuwa katika robo yao ya uwanja walokuwa wanamiliki mpira kwa kupiga pasi huku wakispgea mbele. Walipokuwa wanafika karibu na nusu ya uwanja walikuwa wanapiga mipira mirefu ya moja kwa moja kwa washambuliaji wao. Walijua washambuliaji wao walikuwa na kasi kubwa sana ukilinganisha na mabeki wa...
Kulikuwa na dalili za Mbaraka Yusufu mshambuliaji wa Kagera Sugar kuibuka mchezaji bora wa ligi kuu msimu huu wa 2016-17 lakini kadi nyekundu mechi ya juzi na Yanga SC inamtoa katika kinyang'anyiro hicho . Suala la nidhamu huenda likachafua mbio hizo. Namuona Haruna Niyonzima kurudi kwenye tuzo za mchezaji bora...
Tafadhali tumia viungo rasmi kusambaza habari zetu. Facebook, Twitter au Barua Pepe. Kama utataka kutumia habari zetu tuandikie kupitia habari@kandanda.co.tz