Pamoja na kwamba Kocha mkuu wa Yanga kuonekana kusikitishwa na kiwango cha waamuzi katika mchezo wa jana dhidi ya Mbeya City ambao ilimalizika kwa sare ya 1-1 kocha huyo amegusia kuhusu safu mbovu ya ushambuliaji.
Jana Bernard Morrison aliinusuru timu yake ya Yanga kutofungwa na Mbeya City katika mchezo ambao ulifanyika katika siku ya kuzaliwa kwao wakiwa wanasherehekea miaka 85 tangu timu ianzishwe.