CAF yalia na waandishi wazushi, ni ishu ya Rais Ahmad.
Shirikisho la soka barani Afrika CAF limekanusha taarifa zilizokuwa zikizagaa mitandaoni na kwenye vyombo mbalimbali vya habari barani Afrika kuwa rais wa shirikisho hilo Ahmad Ahmad alinyimwa ruhusa kuingia nchini Marekani. CAF imesema inashangaa kuona taarifa hizo kwani hakukuwa na katazo lolote kwa rais Ahmad na ujumbe wa CAF ambao...