Kupitia mchezo huo Arafat Haji amesema wanauchukua mchezo wa muhimu kwani wanataka kuionyesha Afrika Yanga ni timu ya aina gani na hawataki kupoteza uongozi wa kundi lao.
Endapo Yanga itapata ushindi katika mchezo huo wamwisho kwa wastani mzuri basi watamaliza vinara wa kundi mbele ya US Monastir ambae yeye anamaliza na kibonde Real Bamako.
Yanga si tu walipata ushindi lakini pia walicheza vyema katika dakika zote 90 na kuwadhibiti kabisa Monastir ambao hawakupata hata nafasi yakupiga shuti lililolenga lango.
Mchezo wa mwisho wa kundi hilo Yanga watamalizia ugenini Congo dhidi ya Mazembe hivyo ni vyema leo wakamalizana na Monastir wakiwa nyumbani Kwa Mkapa na kufuzu robo fainali.