Mchambuzi wa mpira wa miguu, mwenye Shahada ya Ualimu. Martin amejiunga na timu ya kandanda toka mwaka 2017, moja kati ya wachambuzi wakongwe katika familia yetu.
Mapinduzi siku zote huja baada ya damu kumwagika. Matokeo mabovu wanayoyapata Simba kwa sasa ni hatua ya wao kufikia mapinduzi ya kweli ya mpira, naamini kuna funzo kubwa wanapata kupitia haya mashindano.
Al Alhly ndiyo mabingwa wa kihistoria wa kombe hili la ligi ya mabingwa barani Afrika. Kombe hili huwa wanalichukulia kwa maanani sana. Siyo rahisi kwao wao kukubali kupoteza nyumbani tena dhidi ya Simba.
Unakumbuka enzi za Boban? Alijua kupiga pasi vizuri, alijua kutengeneza nafasi za kufunga magoli vizuri. Alijua kufunga pia magoli. Alijua kuupaka rangi ya kila aina mpira.
Mtaani kuna picha yako inasambaa sana. Picha ambayo ulipiga kipindi ambacho ndiyo unatua Simba. Kipindi ambacho dunia ya mpira wa miguu ilikufahamu vizuri. Kipindi ambacho kila jicho lilijivunia sana kukuona wewe, hakuna ambaye alikuwa hana furaha kila alipouona mguu wako wa kushoto ukigusa mpira. Kuna wakati hata mashabiki wa Yanga...