Hii ilikuwa lazima ifanyike tena kwa uharaka mkubwa. Ally Salim na Feruz ilikuwa karata ngumu sana kwa Simba SC kuicheza kuelekea Msimu mpya wa mashindano.
Kabla ya mpira kwenda mapumziko Namungo walichomoa bao hilo kupitia kwa Salum Kabunda aliyenufaika na makosa ya Ally Salim kwa kushindwa kuuokoa mpira wa kona vyema uliopigwa na Shiza Kichuya.
Ni wazi Wanasimba wanategemea wachezaji wap kurudia kile kilichotokea miaka 20 nyuma yaani mwaka 2003 ambapo Mnyama alimtoa Zamalek ambae alikua bingwa mtetezi tena katika ardhi ya nyumbani kwake Misri
katika mchezo wa mwaka 2003 langoni alikaa Juma Kaseja na kwa ujasiri mkubwa aliivusha Simba kwa kudaka mikwaju ya penati baada ya matokeo ya sare kwa michezo yote miwili hivyo basi ni Benno ama Salim atapaswa kuvaa viatu vya Manula akiwa na ujasiri wa Kaseja
Katika mchezo huo Yanga walifanikiwa kupiga mashuti sita yaliyolenga lango lakini yote yaliishia mikononi mwa mlinda mlango wa Simba Ally Salim huku Fiston Mayele pekee akipiga mashuti matatu yaliyolenga lango.