Rishald ameongeza kuwa nafasi kubwa ya kuonesha nia ya kutaka kubaki ipo kwenye mchezo wa Jumanne hii dhidi ya Mtibwa Sugar utakaofanyika kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Afisa habari wa Mtibwa Sugar Thobias Kifaru Ligalambwike amesema msafara umeondoka ukiwa na matumaini makubwa ya kuibuka na ushindi katika mchezo huo, ukizingatia mchezo uliopita waliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Azam FC.
Kuelekea mchezo wao wa marejeano wa Caf Confederation Cup dhidi ya KCCA FC ya Uganda kesho Jumamosi, nahodha wa Mtibwa Sugar FC, Shaaban Nditti amekiri watalazimika kucheza 'kufa na kupona' ili kupindua matokeo ya 3-0 na kufuzu kwa hatua ya mwisho kuwania nafasi ya kufuzu kwa hatua ya makundi.
Kiungo mshambulizi wa Mtibwa Sugar FC, Haroun Chanongo amesema wanafahamu wanakabiliwa na kazi kubwa dhidi ya KCCA FC katika mchezo wa kwanza wa raundi ya kwanza ya Caf Confederations Cup.