Shirikisho la soka nchini TFF limethibitisha kuwa michezo miwili ya nyumbani ya African Lyon dhidi ya Simba na Yanga itafanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid uliopo Jijini Arusha.
Klabu ya soka ya Alliance ya jijini Mwanza chini ya kocha Malale Hamsini Keya imeendelea kujifua katika uwanja wa Nyamagana uliopo katikati ya jijini la Mwanza kwa ajili ya michezo ijayo ya ligi kuu soka Tanzania Bara. Malale ambaye hajashinda mchezo wowote toka alipochukua kijiti cha kocha Mbwana Makata aliyetimuliwa...
Habari ambazo zimeenea na viongozi wa Yanga kuwa na kigugumizi kuthibitisha ni kuwa kiungo wa African Lyon na aliyewahi kuchezea Simba, Haruna Moshi "Boban" kuwa amesajiliwa na klabu ya Yanga.
Klabu ya soka ya African Lyon imesema haiwezi kuzungumza lolote kuhusu kuondoka kwa Haruna Moshi Boban ambaye anahusishwa na kujiunga na Yanga SC Kwani bado hawana uhakika na usajili huo na zingine.