Klabu ya soka ya Mbao ‘Wabishi’ umewatoa hofu baadhi ya mashabiki wa timu hiyo, wenye wasiwasi na uwezo wa kocha Ally Bushiri kuwa wanaimani kubwa na kocha huyo kuwa ataleta mafanikio yaliyoachwa na makocha Ettiene Ndayiragije na Amri Said. Msemaji wa klabu hiyo Clisant Malinzi amesema wameuona uwezo wa kocha...
Msemaji wa klabu ya soka ya Mbao ‘Wabishi’ Clisant Malinzi ameutaja mchezo wa Jumamosi hii wa ligi kuu soka Tanzania Bara baina yao na Alliance FC kama dabi ya pili kwa ukubwa Tanzania Bara ukitoa mchezo wa Simba na Yanga. Malinzi amesema kwa kuwa Mwanza ni jiji la pili kwa...
Mashabiki wa Timu ya soka ya Yanga kutoka Tawi la Meatu lililopo wilayani Meatu Mkoani Simiyu wamesema licha ya baadhi ya Mashabiki kutoka timu pinzani kuwabeza kuwa ni ombaomba wanaamini kikosi hicho kilichopo chini ya kocha raia wa kongo Mwinyi Zahera kitachukua ubingwa wa ligi kuu bara msimu wa Mwaka 2018/19.
Kocha mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera amesema shida ambazo klabu hiyo imekumbana nazo ndizo zimewapa morali ya kupambana na kupata matokeo chanya kwenye michezo ya ligi mpaka sasa. Zahera amesema wakiwa kambini mkoani Morogoro kabla ya kuanza kwa ligi alikaa na wachezaji wake na kuwaomba kuungana na kuwa wamoja lakini...
BAADA ya ushindi wa 16 katika michezo 18 ya mzunguko wa kwanza, pointi 50 mabingwa wa kihistoria wa ligi kuu Tanzania bara, Yanga SC wamesema wataifunga pia Azam FC katika mchezo wao wa mwisho wa mzunguko wa kwanza ili kutanua pengo lao la pointi.
Uongozi wa klabu ya soka ya Stand United umelitaka Shirikisho la Kandanda nchini kupitia Bodi ya ligi kuwapatia alama tatu baada ya Alliance kumtumia Bigirimana Blaise kwenye mchezo wao wa ligi siku ya Ijumaa wakati akiwa bado na mkataba na wapiga debe hao. Mwenyekiti Stand United Ellyson Maeja amesema Alliance...
Kocha mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera amekubali ombi la kukutana na baadhi ya wachezaji wa timu hiyo hapo kesho lakini kwa sharti la kutozungumzia suala linalomuhusu mlinda mlango Beno Kakolanya. Zahera ameuambia mtandao huu kuwa alipata taarifa kuwa kuna wachezaji waliowahi kuichezea Yanga wametaka kuzungumza naye lakini katika kudodosa alifahamu...