Licha ya Geita Gold kutangulia kufunga lakini Yanga walitulia na kurudi kwa kasi kipindi cha pili, walirudisha bao hilo na kuongeza mengine na kupata ushindi mnono.
Goli la tatu Baleke alilifunga katika dakika ya 34 kwa kupata pasi ya kichwa kutoka kwa Shomary Kapombe baada ya kuunganisha mpira wa juu uliopigwa na Sadio Kanoute "Putin".
Kwa kufunga mabao hayo matatu "hatrick" anaungana na John Bocco, Fiston Mayele na Ibrahim Mukoko msimu huu ambao nao wamefunga hatrick na kufanya zifike tano msimu huu.
Kikosi cha Simba kimefanya mazoezi yake ya mwisho katika Dimba la Jamuhuri Morogoro kuelekea mchezo wao dhidi ya Mtibwa Sugar utakaopigwa katika Dimba la Manungu.
Baada ya kumaliza majukumu ya Kimataifa katika michezo ya Klabu bingwa kwa upande wa Simba na Shirikisho kwa Yanga na kupata ushindi sasa wanarudi dimbani katika Ligi Kuu ya NBC.
KMC FC itakaporejea mbali na kukutana na Geita Gold Aprili 17 , pia itakuwa na kibarua kingine dhidi ya Dodoma Jiji, Singida Bigi stars, Tanzania Prisons pamoja na Mbeya City